https://www.youtube.com/watch?v=kJro-Uc5TB0
Rais Uhuru Kenyatta amewakemea viongozi wa upinzani kutokana kile alichokitaja kama kuendeleza siasa za kubomoa nchi. Kwenye hotuba yake wakati wa sherehe za kuadhimisha siku kuu ya Jamhuri uwanjani Nyayo, Kenyatta amesema wakati wa kutenganisha wakenya kwa misingi ya kisiasa umekwisha, na yuko tayari kupingwa kwa njia iliyokomaa, na wala sio kwa siasa tu. Kama mwanahabari wetu Kiama Kariuki anavyotueleza, wanahabari pia hawakusazwa kwenye hotuba hiyo, na kila mwanahabari ameonya kuwa ataubeba msalaba wake iwapo ataandika au kupeperusha taarifa za kupotosha.
The post Rais Kenyatta aongoza sherehe za Jamhuri uwanjani Nyayo appeared first on Mediamax Network Limited.